SW/Prabhupada 0028 - Buddha is God

Revision as of 05:15, 12 July 2019 by Vanibot (talk | contribs) (Vanibot #0023: VideoLocalizer - changed YouTube player to show hard-coded subtitles version)
(diff) ← Older revision | Latest revision (diff) | Newer revision → (diff)


Lecture on Sri Isopanisad, Mantra 1 -- Los Angeles, May 3, 1970

Gargamuni: (kusoma:) "Ni makosa pia kuwa mlaji mboga pekee tu mtu anaweza jiokoa kutokana na kupita katika sheria za maumbile. Mboga pia zina uhai. maisha ya kiumbe mmoja inamaanisha kukula viumbe wengine, na hii ndio sheria ya maumbile. Mtu hafai kujivunia kwa kuwa mlaji mboga mkali. hatua ni kumtambua Mungu Mkuu. Wanyama hawana ufahamu uliokomaa kiwango cha kumtambua Mungu kama binadamu..."

Prabhupāda: hii ndio hatua muhimu. kama vile Wabuda, pia wao ni walaji mboga. Kulingana na kanuni za Wabuda... Siku hizi kila kitu kimeharibika, lakini mtangazo wa Mola Buda ilikuwa kufanya wajinga kuacha mauaji ya wanyama. Ahiṁsā paramo dharma Kukuja kwa Mola Buda kumeelezwa katika Śrīmad-Bhāgavatam na maandiko mengine ya kiVeda. Sura-dviṣām Alikuja kudanganya mapepo. Mapepo...Aliweka sera hivi kwamba mapepo walidanganyika. Amewadanganyaje? Mapepo, wako kinyume na Mungu. Hawaamini Mungu. Hivyo Mungu Buda alieneza, "Ndio, hakuna Mungu. Lakini vile nasema, ufuate." "Ndio, bwana." Lakini yeye ni Mungu. Hii ni udanganyaji. Ndio. Hawaamini Mungu, lakini wanaamini Buda, na Buda ni Mungu. Keśava-dhṛta-buddha-śarīra jaya jagadīśa hare. Hivyo hii ndio tofauti kati ya mapepo na muumini. Muumini huwa anaona vile Kṛṣṇa, Keśava, anadanganya wajinga hawa. Muumini anawezaelewa. Lakini mapepo, wanafikiria, "Ah, tuko na kiongozi mzuri. Haamini Mungu." (kicheko) Unaona? Sammohāya sura-dviṣām (SB 1.3.24). Jina kamili la Kisanskriti imesemwa kwa Śrīmad-Bhāgavatam. Umeona, wale wamesoma: sammohāya, kwa kuchanganyisha sura-dviṣām. Sura-dviṣām inamaanisha watu ambao wenye wivu kwa waumini. Kafiri, mapepo, wanawaonea wivu waumini kila mara. hiyo ndio sheria ya maumbile. Unaona baba huyu. Baba alikuwa adui ya mtoto wake kijana wa miaka tano. Nini ilikuwa makosa yake? Alikuwa muumini. Hivyo tu. Kijana asio na hatia. Alikuwa , namaanisha kusema,alivutiwa na kukariri kwa Hare Kṛṣṇa mantra. Babake mwenyewe, alikuwa adui sugu: "Ua kijana huyu," Hivyo kama baba anawezakuwa adui, na wengine. hivyo unapaswa kutarajia kwamba mara tu umekua muumini, dunia yote inakuwa adui. Hiyo tu. Lakini lazima ukabiliane nao, kwa sababu umeamuliwa kama mtumishi wa Mungu. misheni yako ni kuwaangazia kimafunzo. Hivyo hauwezi. Kama Mungu Nityānanda, Aliumizwa, lakini bado aliokoa Jagāi-Mādhāi. Hio ndio inafaa kuwa kanuni. wakati mwingine lazima tudanganye, wakati mwingine lazima tuumizwe, vitu nyingi sana. Kifaa pekee tulichonacho ni vile watu wanaweza mfahamu Kṛṣṇa. Hiyo ndio dhamira yetu. Kwa njia moja au nyingine hawa wajinga wanapaswa kubadilishwa kuwa wafahamu wa Kṛṣṇa, aidha kwa njia hii ama nyingine.