SW/Prabhupada 1066 - Watu wenye akili duni wanadhania kuwa Mwenyezi Mungu hana utu



660219-20 - Lecture BG Introduction - New York

Kwa hivyo mpangilio wate ni kuwa kuwa mfaidi ni Mwenyezi Mungi, na viumbe vyote wanashirikiana naye tu. Katika huo ushirikiano, vina faidi. Huo uhusiano bi kama vile ya Bwana na mtumishi wake. Ikiwa Bwana ameridhika kabisa mtumishi wake pia bila shaka ataridhika. Hio ni sheria. Vile vile, Mwenyezi Mungu anapaswa kuridhika, tabia ya kujifanya waumba au wenye kufaidi katika hii dunia ipo ndani ya viumbe vyote kwa sababu ipo ndani ya Mwenyezi Mungu. Ameumba ulimwengu mzima.

Kwa hivyo kwenye Bhagavad-gītā tutaona kwa jumla kuwa Mtawala mkuu, viumbe watawaliwa, ulimwengu mzima, muda uishie milele na vitendo, vyote vimeelezwa. Kwa hivyo hayo yote kwa jumla yanaitwa, Ukweli Ulio timilika. Ukeli huu ulio timlika basi ndiyo yeye Mungu Mkuu Śrī Kṛṣṇa. Kama vile nimeeleza kuwa udhiirisho zinatokana na nguvu tofauti, na yeye ndiye jumla yote kamili.

Imeelezwa kwenye Bhagavad-gītā kuwa Brahman asiye na utu pia ni yuko chini ya mtu aliye timilika. Brahmaṇo 'haṁ pratiṣṭhā (BG 14.27). Brahman asiye na utu pia imeelezwa kwenye Brahma-sūtra kuwa yeye ni nuru. kama vile kuna nuru ya jua au jua kama sayari, vile vile, Brahman asiokuwa na utu ni kama nuru zinazo angaza zake Brahman Mkuu au Mwenyezi Mungu aliye na utu. Kwa hivyo Brahman asiyo na utu ni utambuzi wa Ukweli Mkuu usiotosha, na pia ule utambuzi wa Paramātmā yameelezwa. Puruṣottama-yoga. Tutakapo soma katika sura ya Puruṣottama-yoga tutaona kuwa, Mungu Mkuu au Puruṣottama, yu juu ya Brahman na utambuzi mdogo wa Paramātmā. Mungu Mkuu anajulikana kama

sac-cid-ānanda-vigrahaḥ (BS 5.1). kwenye Brahma-saṁhitā, mwanzo umaanzwa hivi: īśvaraḥ paramaḥ kṛṣṇaḥ sac-cid-ānanda-vigrahaḥ/ anādir ādir govindaḥ sarva-kāraṇa-kāraṇam (BS 5.1)."Govinda, Kṛṣṇa, ndiye sababu ya sababu zote. Yeye ndiye Bwana Mkongwe." Kwa hivyo Mungu Mkuu yu sac-cid-ānanda-vigrahaḥ. Brahman asiye na utu ni utambuzi wa kiungo chake cha sat yaani anayeishi milele. Na utambuzi wa Paramātmā ni utambuzi ambao ni wa viungo vya sat-cit, yaani aishiye milele na pia mwenye maarifa yote. Lakini utambuzi wa Utu wa Mungu kama Kṛṣṇa ni utambuzi wa viungo vyake vyote takatifu kama vile sat, cit, and ānanda yenye vigraha kamili. Vigraha inamaanisha umbo. Avyaktaṁ vyaktim āpannaṁ manyante mām abuddhayaḥ (BG 7.24). watu wenye akili duni, wanadhani kuwa Mwenyezi Mungu hana nafsi, walakini yeye ni mtu, mtu mtakatifu. Hiyo ime tibitishwa kwenye vitabu vyote vya Vedasi. Nityo nityānāṁ cetanaś cetanānām (Kaṭha Upaniṣad 2.2.13). Kwa hivyo sisi pia ni watu, viumbe binafsi, sote tuna nafsi zetu vile vile, Mweyezi Mungu pia mwishowe ni Mtu. lakini utambuzi wa kweli wa Mwenyezi Mungu ni ule utambuuzi wa maumbile yake yote takatifu kama vile sat, cit, and ānanda, kwenye ukamilifu wa maubile yake. Vigraha inamaanisha umbo. Kwa hivyo Jumuia kamili ina umbo. ikiwa hana umbo, au ni duni kuliko vitu vyote vinginevyo. hawezi kuwa Jumuia kamili. Jumuia kamili lazima imiliki vitu vyote ambavyo viko kwenye uzoefu wetu na pia zaidi ya uzoefu wetu. Au sivyo, haiwezi kutimilika. Jumuia Kamili yaani Mwenyezi Mungu anamiliki nguvu nyingi ajabu. Parāsya śaktir vividhaiva śrūyate (CC Madhya 13.65 ). hayo pia yameelezwa kwenye Bhagavad-gītā, yani vile anavyo tena kupitia nguvu tofauti. pūrṇam idam ( kiazio cha Śrī Īśopaniṣad,). Dunia tuliyowekwa pia ina inaukamilifu wake kwa sababu vile vipengele ishirini na nne ambayo kulingana na falsafa ya Sāṅkhya, yana sababisha udhiirisho wa ulimwengu huu kwa muda mfupi, yameundwa kuzalisha vitu kamilifu ambavyo yana hitajika kudmisha madutu ya ulimwengu huu. hakuna juhudi ya kitu chochote inahitajika kudumisha ulimwengu huu. Imeunganishwa na nguvu za Jumuia nzima, na wakati unapotimia, udhirisho huu uliyo wa mda mfupi, itaangamizwa na mpangilio wa mkamilifu.